AHADI ZOTE ZA MUNGU ZINASIMAMA KWELI (KMC)
1. Ahadi zote za Mungu zinasimama kweli, na
zilitiwa muhuri kwa damu yake Yesu.
Ref. : Mbingu zikiondoka, nchi ikitoweka,
aminiye taona: ahadi zinadumu.
2. Fanya kama Ibrahimu: Uangalie juu!
Nyota ukizihesabu, imani itaota.
3. Katika giza njiani tutaamini tu.
Muda kitambo, na tena jua litaangaa.
4.Watu wakitusumbua, tutaamini tu.
Yesu atusaidia majaribuni pote.
5. Rafiki wakituacha, tutaamini tu.
Yesu rafiki, mkubwa, atabaki daima.
6. Katika mambo yo yote tutaamini tu.
Tutaviona mbinguni tulivyoviamini.
Ещё видео!