Tunda la parachichi au kunywa juisi yake mara nyingi hujulikana kama chakula chenye afya.Hivyo Umaarufu wa parachichi unatokana na umbile lake nyororo, laini na ladha isiyo ya kawaida. Parachichi ni tunda ambalo ni la familia ya mdalasini. Kuna aina kadhaa ya parachichi, kuanzia ukubwa, rangi na muundo.
Lakini pia Yote yanakuwa katika asili ya hali ya hewa ya kitropiki na yanapovunwa, ni nyororo na laini kama siagi ambapo yamekuwa maarufu sana katika kila kitu kuanzia kwenye kuchanganyia kwenye mlo mpaka kula baada ya chakula.
Pia Ni kweli kwamba tunda hili lina mafuta, ingawa lina virutubisho, madini na sifa ambazo ni muhimu sana kwetu.Ndani ya tunda hili kuna maji kiasi kidogo sana ukilinganisha na matunda mengine lakini kuna mafuta mengi lakini pia unaweza kuchanganya kwa kula na matunda mengine kama vile apple, ndizi, chungwa au hata maziwa kwa kutengeneza juisi.
Licha ya kuwa na mafuta parachichi lina tindikali yaani acid mbalimbali ikiwemo inayojulikana kama amino ambayo husaidia sana kukinga na kutibu maradhi katika mwili wa binadamu. Tunda hili pia lina protini ya kiwango cha juu.
Pia kuna tindikali inayoitwa oleic acid OLIEKI ACID kwenye parachichi ambayo husaidia kukinga magonjwa ya moyo, kiharusi na kansa.
Ещё видео!