MAHAKAMANI
NA MERCY SEKABOGO
July 12, 2017
SONGWE
TV/PRESS
JELA MAISHA KWA KULAWITI
MAHAKAMA ya wilaya ya Momba mkoani Songwe imemhukumu kutumikia kifungo cha maisha kijana aliyejulikana kwa jina la Duma Lundilo Pangarasi, mkazi wa Isanzo Chunya mkoani Mbeya kwa kosa la Kubaka na kulawiti mtoto wa kiume mwanafunzi wa darasa la tatu wa shule ya msingi Mbao iliyopo Wilayani Momba.
Duma Ludilo Pangarasi mwenye miaka 26, alikuwa akikabiliwa nakesi ya jinai namba 196 / 2016, shauri ambalo lilifikishwa mahakamani hapo mnamo Novemba 8 /2016 Mbele ya hakimu Mfawidhi Zabibu Mpangule akituhumiwa kumlawiti mtoto huyo kinyume cha sheria 154/kifungu cha kwanza A na cha pili kanuni ya adhabu sura 16 ya sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Ilielezwa mahakakani hapo na mwendesha mashtaka wa polisi Leonard Mwamafupa mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Wiaya James Mhanusi kuwa shahidi wa kwanza ambaye ni mtoto aliyelalawitiwa aliieleza mahakama kuwa mnamo Nove 7 2016 muda wa mchana akitoka shule alichomwa na mwiba katika harakati za kuchomoa mwiba katika kiatu chake alikurupushwa na mtu aliyetoa kichakani akiwa na fimbo mkononi na kumtaka asikimbie vinginevyo angemuua .
Baada ya kusimama aliamuriwa kuvua nguo zote mtoto alitii na kisha Pangarasi alitekeleza tendo hilo la kinyama na alipotosheka akamwacha aende zake, mtoto huyo alipofika kwa mzazi wake alimweleza huku akimtaja mtuhumiwa kwa jina la msukuma mchunga Ng’ombe alimfanyia machafu hayo.
Mbele ya mahakama mshtakiwa aliwahi kuomboleza kuwa adhabu aliyopata gerezani imemtosha kujifunza hivyo aachiwe kwani hawezi rudia kutenda kosa kama hilo, kauri iliyoashiria ukiri wa shitaka, maombolezo ambayo yameifanya mahakama kuridhishwa na mashahidi waliotoa ushahidi mahakamani hapo akiwemo mzazi pamoja na daktari Stanrey Simbeye ambaye alipokea mtoto huyo kwaajili ya matibabu.
Aidha kabla ya kutoa adhabu hiyo Hakimu Mhanusi amemtaka mshtakiwa ajitete kwani mahakama imemtia hatiani, ndipo mshtakiwa alipoiomba mahakama isimpasie adhabu kali kwani yeye ni muathirika wa ugonjwa wa Ukimwi lakini pia anafamilia inayomtegemea ombolezo ambalo limetupiliwa mbali na mahakama na kumhukumu kutumikia kifungo cha maisha Jela ili iwe fundishisho kwa watu wengine.
Sign off
![](https://i.ytimg.com/vi/0SnpQl0U5yU/maxresdefault.jpg)