Mbunge wa Viti Maalumu kundi la watu wenye ulemavu, Khadija Taya (Keisha) ameomba mwongozo wa kiti cha spika kutaka kujadili juu ya kifo cha mtoto mwenye ualbino Asimwe Novath ambaye alinyakuliwa na watu wasiojulikana na kukutwa amefariki baada ya siku 19.
Keisha ameomba mwongozo wa Bunge, ili wabunge wajadili kuhusu jambo hilo, ila Naibu spika alimuomba kwenda kuonana na Waziri wa Mambo ya Ndani ili kupata utaratibu mzuri wa jambo hilo.
![](https://i.ytimg.com/vi/1XWoEAvhuuQ/maxresdefault.jpg)