Albert Mrema aliyenusurika katika ajali ya gari iliyosababisha vifo vya mama na wanawe wawili, naye amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo.
Mrema aliyekuwa kuwa anaendesha gari iliyopoteza uelekeo na kuangukia kwenye bonde na kusababisha kifo cha mama yake Immaculata Byemerwa na wadogo zake wawili Jolister Byemerwa na Janeth Byemerwa waliozikwa jana , toka siku ya ajali hiyo iliyotokea Novemba 26, 2022 alikuwa amelezwa kwenye chumba cha ungaliazi maalumu katika hospitali ya Mloganzila akipatiwa matibabu.
Taarifa za kifo hicho ambacho kinaendelea kuhumiza familia hiyo imethibitishwa na mdogo wa marehemu huyo Prince Byemerwa leo Disemba 2,2022 ambaye amesema "Nikweli kaka yangu amefariki Dunia toka jana jioni hospitali ya Mloganzila alilkokuwa akipatiwa matibabu''
Ещё видео!