Bint anayefahamika kwa majina Wendi Mrema anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 40 Mkazi wa Kijiji cha Rau Wilayani Moshi Mkoani Kilimanjaro anatuhumiwa kumuua mama yake Mzazi Patricia Ibreck mwenye umri wa miaka 66 kwa kushirikiana na Waganga wawili wa kienyeji huku kwa pamoja wakichimba shimo na kuzika mwili kwa siri kwa madai ya tamaa za mali mkoani humo.
Ikiwa ni zaidi ya miezi kumi toka mwili huo ukiwa ardhini kwa usiri, ndugu walipotaka kujua Patricia yupo wapi mtuhumiwa aliwalijibu kuwa Mama yake yupo India kwa ajili ya kutibu afya yake na fedha lukuki zinahitajika kwa ajili ya matibabu.
Awali ya tukio hilo inaelezwa kuwa Mama mzazi wa Wendi aliugua na alianza kupatiwa matibabu na Waganga wa kienyeji waliokuwa wameletwa mtuhumiwa ambaye ni mtoto wa kumzaa, na alipoona haponi alianza kupata mashaka kuwa kuna utapeleli unaendelea ukiongozwa na mwanae kwakushirikiana Waganga huku akiwa ameshatumia milioni 60 kwa ajili ya matibabu, na hapo ndipo mabishano yalianza na kundi hilo kudaiwa kumuua na kumzika kwa usiri na maeneo kuanza kuuzwa huku binti akiambia famila kuwa Mama yake yupo India na amesema maeneo yauzwe ili atumiwe fedha za matibabu.
Hata hivyo mmoja wa mwanafamilia ametueleza kuwa Marehemu alikuwa anasumbuliwa na tatizo la miguu na mara nyini alionekana akichechemea.
Kwa upande wa jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limelazimika kufukua shimbo lililokuwa limetumika kumficha
#gaditv #breakingnews #updates #mauajiMoshi
#Kilimanjaro
GADI TV ndiyo
Channel pekee inayokuwezesha kupata Habari za Kisiasa,Michezo, Kijamii, na Burudani kutoka Ndani na Nje ya Tanzania. Kwa huduma ya Matangazo au Habari pamoja na maoni na ushauri usisite kuwasiliana nasi kupitia namba za simu +255 769 780 063 au e-mail: gaditvhabari@gmail.com
Don't forget to SUBSCRIBE, LIKE, COMMENT and SHARE!!! # GADI TV
Thanks.
![](https://i.ytimg.com/vi/2OV4pegHPAg/maxresdefault.jpg)