Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip
Mpango amesisitiza umuhimu wa wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii
kuwasaidia wananchi kwa kutoa elimu kuepukana na maradhi mbalimbali.
Makamu wa Rais ametoa wito huo mara baada ya kutembelea Zahanati ya
Kijiji cha Kasumo akiwa wilayani Buhigwe mkoani Kigoma. Amesema maradhi
yanayotajwa kuwasumbua wananchi wa Kijiji hicho ikiwemo magonjwa ya
mfumo wa hewa pamoja na magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji yasio salama yanaweza kudhibitiwa kwa kutoa elimu kupitia mikutano mbalimbali ya Kijiji.
Amewahimiza wahudumu wa afya ngazi ya jamii kuwatembelea wanakijiji
katika maeneo yao na kuwaelimisha namna ya kuwalinda watoto dhidi ya
michezo katika maji machafu pamoja na unywaji maji yasiochemshwa.
Amewataka wananchi wa Kijiji hicho kuweka utaratibu wa kuchemsha maji
kabla ya kunywa na kuondokana na imani waliyonayo kwamba maji ya
kuchemsha sio matamu.
Makamu wa Rais amewapongeza wanakijiji hao kwa kwa kujitoa katika
kukamilisha zahanati hiyo ambayo imekua msaada kwa wananchi wa Kijiji
hicho na vijiji Jirani.
#kahitila255
Ещё видео!