Na Joel Maduka, Geita
Baraza Kuu la Waislamu (BAKWATA) mkoani Geita linatarajia kuanza ujenzi wa jengo la ghorofa nne litakalogharimu zaidi ya shilingi biloni tatu ambapo litakuwa na Msikiti, maduka zaidi ya 100, kumbi za mikutani pamoja na vyumba vya kulala wageni.
Mwenyekiti wa Baraza hilo, Alhaji Said Karidushi amesema kuanzishwa kwa miradi hiyo kutafungua mwanya mkubwa wa kuwasaidia watu mbalimbali hususani katika sekta ya elimu na afya.
Karidushi amesema pia Baraza hilo linatarajia kujenga Chuo cha Mafunzo kitakachowahudumia wanajamii kutoka dini zote.
Naye Sheikh Mkuu wa Mkoa Geita, Alhad Yusuf Kabaju amesema miradi hiyo inatarajiwa kuanza mwaka huu na kukamilika kwa wakati kwani lengo ni kuhakikisha BAKWATA inakua kiuchumi na kutimiza malengo yake.
Ещё видео!