Wabunge na maseneta kufikia sasa hawajapokea mshahara wao wa mwezi aprili, huku vuta nikuvute kati yao na tume ya mishahara ikizidi kushamiri. Wabunge wamesusia kupokea malipo yao, huku wakizidi kushinikiza tume ya Sarah Serem ibatilishe pendekezo la kupunguza mishahara ya wabunge kutoka shilingi laki nane unusu, hadi shilingi laki tano na elfu arobaine. Katibu wa bunge Justin Bundi amedhibitisha kuwa wabunge bado hawajapata hela zao, huku akifichua kuwa tume ya kuwaajiri wafanyi kazi wa bunge(PSC) inazidi kushauriana na tume ya mishahara.
![](https://i.ytimg.com/vi/4lh0MOozVEw/maxresdefault.jpg)