WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na maboresho yaliyofanyika katika hospitali ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa Oktoba 18, 2022 alipofanya ziara hospitalini hapo.
Mheshimiwa Waziri Mkuu alipofanya ziara katika hospitali hiyo na alieleza kutorishwa na milango iliyowekwa na kuagiza iondolewe na iwekwe mingine yenye viwango na leo Januari 06, 2023 amekagua maendeleo ya utekelezaji wa agizo na ameridhishwa na kazi iliyofanyika.
Kufuatia utekelezaji huo Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na utekelezaji wa maelekezo hayo ambapo hadi sasa jumla ya milango 67 kati ya 84 imeondolewa na kuwekwa mipya yenye ubora.
“Leo nimeona milango bora kabisa, kwa nini tulikubali kuweka milango mibovu wakati mizuri ipo? Hii haikubaliki kwa sababu tunapoteza fedha za Serikali zinazotokana na kodi ya wananchi. Ni lazima kila mtumishi wa umma atimize wajibu wake.”
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: [ Ссылка ]...
HabariLeo: [ Ссылка ]
DailyNews: [ Ссылка ]
INSTAGRAM;
HabariLeo: [ Ссылка ]...
SpotiLeo: [ Ссылка ]...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: [ Ссылка ]
Ещё видео!