Moshi. Hatua ya Manispaa ya Moshi kutupwa namba za chini katika mashindano ya usafi miongoni mwa manispaa na majiji nchini, imeilazimisha manispaa hiyo kuja na mkakati mpya wa kuwatumia madereva wa pikipiki kukabiliana na wachafuzi wa mazingira.
Akizungumza kwa niaba aya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, David Kimaro ambae ni ofisa mazingira, amesema sheria zinaeleza atakayetupa taka adhabu faini ni Sh50 000, hivyo kwa yeyote atakayekamata mtu aliyetupa taka atapewa asilimia 50 ya fedha hizo (Sh25,000).
Amesema sheria hiyo si ngeni na watatoa vitambulisho maalumu kwa madereva hao ili akimshika mtu iwe rahisi kutambulika kuwa amepewa jukumu la utunzaji usafi katika manispaa hiyo.
Manispaa ya Moshi ipo katika juhudi za kurejesha heshima ya usafi ya mji ili kuendelea kuwa kinara kitaifa.
![](https://i.ytimg.com/vi/5RpafuZWcfA/maxresdefault.jpg)