Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila ameyasema hayo mapema leo Juni 23,2024 Kufuatia uwepo wa taarifa za uvumi wa mgomo wa wafanyabiashara wa kariakoo ambapo amewataka wafanyabiashara kuepuka kushiriki kwenye masuala yanayoweza kuleta uvunjifu wa amani na kurudisha nyuma uchumi ikiwemo mgomo huu kwani Serikali imeshashughulikia baadhi ya changamoto na inaendelea kushughulikia changamoto za wafanyabiashara hususani zile zinazohusu mabadiliko ya Kisheria.
RC Chalamila amewataka wafanyabiashara kutambua kuwa mgomo sio suluhisho pekee la kutatua changamoto bali utaratibu bora wa kutatua changamoto ni kukaa mezani na mamlaka kujadili kwani mgomo huongeza chuki na wakati mwingine kusababisha uvunjifu wa amani.
#sports #entertainment #BONGONEWSTV Usisahau ku-subscribe channel hii kwa taarifa nyingi zaidi na pia tembelea mitandao yetu ya kijamii Instagram @bongonewstz twitter @bongonewstz na Facebook @bongonewstz
![](https://i.ytimg.com/vi/5YosxyQJJaY/maxresdefault.jpg)