Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoa wa Arusha kuanza uchunguzi dhidi ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Injinia Juma Hamsini na baadhi ya wasaidizi wake kutokana na kukabiliwa na tuhuma za rushwa na ubadhirifu wa fedha za walipa kodi.
Mhe. Mkuu wa Mkoa amechukua hatua hizo baada ya Mwenyekiti wa waongoza watalii mkoa wa Arusha Wilbard John Chambulo kudai kuwa baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha wamekuwa wakitengeneza nyaraka bandia pamoja na kuchepusha baadhi ya makusanyo ya kodi zinazotokana na sekta ya Utalii.
#tbr24media #tabora #rushwa #arusha #makonda #utalii #tanzania
![](https://i.ytimg.com/vi/6g2IOauOZZU/mqdefault.jpg)