#breakingnews #raissamia #vyamavyasiasa#mnyikajohn#chadema
Muungano wa vyama vya siasa vya upinzani nchini umemuomba Rais Samia Suluhu Hassan aharakishe utengenezaji wa kanuni za mikutano hiyo ya hadhara pamoja na masuala ya ruzuku ya vyama vya siasa ili waweze kujiendesha na wananchi waone sera zao.
Aidha muungano huo umetangaza kuunga mkono ripoti ya Kikosi cha kazi kilichoundwa na Rais Samia kutafuta na kuchakata maoni ya wadau kuhusu mfumo wa demokrasia, huku wakikosoa msimamo wa Chadema kupinga ripoti hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Katibu Mkuu wa Chama cha Aliance For Democratic Change (ADC) Doyo Hassan alisema kama nchi itakuwa na vyama vya siasa ambavyo vimeimarika vizuri na ni wazi kuwa maendeleo ya nchi na wananachi yataonekana.
“Leo vyama vya siasa vinaonekana vimedumaa kwa sababu ya uchumi wa fedha, lakini leo Rais amelisikia hilo kupitia kikosi kazi hivyo tunaomba lifanyie kazi haraka ili tuweze kufanya siasa kwa raha na amani,”
Ещё видео!