Makanisa sasa yanamtaka Rais William Ruto kusikiliza na kuchukua hatua dhidi ya malalamishi yanayotolewa na wakenya na kusababisha maandamano nchini. Makanisa yakiongozwa na kanisa katoliki yanamtaka Rais Ruto kuratibu mikakati itakayosaidia kupunguza matumizi ya serikali na kuwakabili viongozi wafisadi. Haya yamejiri huku baadhi ya makundi ya kidini yakitaka kupigwa marufuku kwa wanasiasa kuzungumza makanisani, Kama Brenda Wanga anavyoarifu
![](https://i.ytimg.com/vi/8qgbzLO8Bgc/maxresdefault.jpg)