MTWARA : MAAFISA WA POLISI, WALIOMUUA MFANYABIASHARA WA MADINI WAFIKISHWA KIZIMBANI
Maafisa saba wa Jeshi la Polisi wanaotuhumiwa kumuua mfanyabiasha wa madini, Musa Hamisi, aliyekuwa mkazi wa Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara na shtaka lao kupangiwa tena tarehe nyingine, ambayo ni Juni 16 mwaka huu, kwa ajili ya kusikilizwa.
Watuhumiwa wote wamerudishwa rumande baada ya Mwendesha Mashtaka wa Jamhuri, Severine Mganga kuieleza mahakama kwamba upelelezi wa shtaka hilo bado haujakamilika.
#Mtwara #Mauaji #businessnews
Ещё видео!