Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana katika kikao chake maalumu leo October 01, 2023, Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wake na Rais Samia Suluhu Hassan imefanya uteuzi wa Makatibu Wakuu wa Jumuiya za Umoja wa Wanawake (UWT) na Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM).
Kamati hiyo imemteua Jokate Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa UWT ambapo kabla ya uteuzi huo Jokate alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Tanga.
Kamati Kuu imemteua pia Fakii Raphael Lulandala kuwa Katibu Mkuu wa UVCCM, kabla ya uteuzi huo Lulandala alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Momba, Mkoani Songwe.
Katika hatua nyingine Kamati imemtea Hamad Khamis Hamad, kuwa Mgombea wa CCM wa nafasi ya Uwakilishi katika Jimbo la Matembwe.
![](https://i.ytimg.com/vi/ALebIg5Eerc/maxresdefault.jpg)