Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameieleza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuwa wizara yake imekutana na mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa kanda ya Tanzania na Benki hiyo imekubali kuongeza kasi ya utoaji fedha za ujenzi wa uwanja wa ndege wa Msalato - Dodoma ili uweze kukamilika ifikapo Disemba mwaka huu.
![](https://i.ytimg.com/vi/AZAjoCMAY5o/maxresdefault.jpg)