Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wanne akiwemo Askari Polisi mmoja namba G.8695 PC JOHN KAIJAGE [34] Mkazi wa Isyesye Jijini Mbeya, kwa tuhuma za kumuua ERASTO MWALWEGO [29] Dereva Pikipiki Maarufu kama Bodaboda ambae ni Mkazi wa Nzovwe jijini Mbeya .
Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya Urlich Matei amesema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 21:00 Usiku huko katika nyumba ya kulala wageni iitwayo “The Governor City Lodge” iliyopo Iwambi Jijini Mbeya ambapo watuhumiwa walimshambulia ERASTO MWALWEGO [29] Dereva Bodaboda Mkazi wa Nzovwe sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kitu butu.
Ещё видео!