MwenyeKiti wa Kamati ya Bajeti Ndindi Nyoro amewahakikishia wakenya ya kuwa serikali itatilia maanani Maoni yao kuhusu bajeti na mswada wa fedha wa mwaka 2023. Akizungumza wakati wa ibada ya shukrani katika kanisa la ACK Ndutumi , Nyoro amesema bajeti imetilia uzito masuala ya Masomo, miundo msingi , kilimo na Afya miongoni mwa sekta zingine ili kubadili maisha ya wananchi. Gavana wa Murang'a Irungu Kang'ata ameitaka Serikali kusambaza mgawo wa fedha kwa Kaunti haraka ili kuwezesha kaunti kutimiza majukumu yake.
Ещё видео!