MSIGWA WA CHADEMA AHAMIA CCM
Mwanachama Mwandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mchungaji Peter Msigwa amejiunga rasmi na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mchungaji Msigwa amepokewa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Samia Suluhu Hassan.
Mchungaji Msigwa alizaliwa Juni 8 1965, ni mwanasiasa Mtanzania aliyewahi kuwa Mbunge wa Iringa Mjini (2015-2020) kwa Chama cha Chadema.
Mei 30, 2024 Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alimshinda Mchungaji Msigwa kwenye Cheo cha Uwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Nyasa.
Katika uchaguzi wa kanda hiyo uliofanyika ukumbi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Makambako, ambao ulikuwa na mchuano mkali, Sugu aliibuka kidedea baada ya kupata kura 52 sawa na asilimia 51 dhidi ya Mbunge wa zamani wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa aliyepata kura 51 (asilimia 49).
Matokeo hayo Mchungaji Msigwa hakukubaliana nayo kwa kile alichodai haki haikutendeka na alikata rufaa.
![](https://i.ytimg.com/vi/CoXCZ0KgL4c/maxresdefault.jpg)