WATOTO WAWILI WA FAMILIA MOJA MULEBA WAFARIKI KWA KUUNGUA NA MOTO NDANI YA NYUMBA
Watoto wawili wa familia moja katika Kitongoji cha Kyajoshwa Kijiji cha Kanyamika Wilayani Muleba Mkoani Kagera wamekutwa wamefariki kwa kuungua na moto wakiwa ndani baada ya nyumba yao kuungua moto na chanzo cha tukio kikiwa hakijatambulika.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kyajoshwa Bw. John Bakilana amewataja watoto hao kuwa ni Mariam Mateso mwenye umri wa miaka miwili na Laulent Mateso mwenye umri wa miaka mitatu na ambapo tukiohilo limetokea july 2 majira ya jioni wakati baba yao mazazi akiwa mtoni anateka maji.
Bw. Bakilana amesema kuwa tukio hilo nila mara ya pili ndani ya familia hiyo ambapo tukio la kwanza lilitokea june 28 mwaka huu wakiwa ndani wamelala lakini walitoka wakiwa salama ndipo likatokea tukio hilo na kuua watoto hao ambalo chanzo chake hakijajulikana.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Muleba Dkt. Abel Nyamahanga ameagiza jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina na kwa wakati kujua chanzo cha tukio hilo huku akiwataka wananchi kuwa na subra na kutojichukuria sheria mkononi kwa kutuhumu mtu ambaye hana hatia na kusababisha uvunjifu wa amani.
Aidha jeshi la polisi Wilayani humo limefika eneo la tukio na kuruhusu taratibu za mazishi ziendelee.
Ещё видео!