Washtakiwa watatu kati ya wanne walioshtakiwa kwa kosa la mauaji ya Milembe Suleiman (43), aliyekuwa mfanyakazi wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) wametiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa.
Mahakama imetoa adhabu hiyo baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri ambao umethibitisha kosa hilo pasipo kuacha shaka.
Hukumu hiyo imetolewa leo Jumanne Agosti 27, 2024 kuanzia saa 3.02 asubuhi hadi saa 5.12 asubuhi na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Geita, Kelvin Mhina.
Jaji Mhina aliyesikiliza kesi hiyo amesema kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri, Mahakama imewatia hatiani washtakiwa wa kwanza hadi wa tatu na kumuachia huru wa nne, Musa Lubingo.
Waliotiwa hatiani katika kesi hiyo ya jinai namba 39 ya mwaka 2023 ni mshtakiwa wa kwanza, Dayfath Maunga (30), wa pili ni Safari Lubingo (54), na wa tatu ni Genja Pastory.
Ещё видео!