Bodi ya Ligi imetangaza rasmi kuwa Ligi Kuu Tanzania Bara itakuwa na timu 16 katika msimu wa mwaka 2021/22.
Afisa Mtendaji Mkuu wa bodi hiyo Boniface Wambura amesema kabla ya kufikia timu 16, ligi hiyo itakuwa na timu 18 msimu wa 2020/21 baada ya msimu huu wa 2019/20 kumaliza na timu 20.
Wambura amefafanua jinsi timu zitakavyokuwa zikishuka daraja pamoja na mabadiliko mengine kwenye Ligi Daraja la Kwanza.
![](https://i.ytimg.com/vi/F3l5on-qiWk/maxresdefault.jpg)