DAR ES SALAAM: JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata na kumuhoji kwa kina Khamis Bakari, Mkazi wa Temeke kwa tuhuma za mauaji ya A bdallah Twahir Selemani ambaye alikuwa rafiki yake na baada ya kumuua alifanikiwa kuiiba pesa za marehemu shilingi Milioni 61 kutoka kwenye akaunti ya huyo rafiki yake.
Akizungumza na waandishi wa Habari, Kamanda wa polisi wa kanda hiyo, SACP. Jumanne Muliro amesema majira ya saa 10:20 asubuhi huko maeneo Mbutu Kichangani, Kigamboni pembezoni mwa barabara itwayo Cheka kuelekea beach ya Kichangani uliokotwa mwili wa mtu mmoja mwanaume akiwa ameshafariki na baadae mwili huo ulitambuliwa kuwa ni Abdallah Twahir Selemani mkazi wa Chanika.
"Jeshi la Polisi lilipokea taarifa ya kupotea kwa Abulllah Twahir Selemani kutoka kwa mama yake kuwa alipotea katika mazingira ya kutatanisha. Uchunguzi wa Jeshi la Polisi baadae uligundua kuwa tarehe 30 Aprili 2024 mtuhumiwa Mussa Khamis Bakari alikuwa na marehemu wakitumia gari namba T.928 DFY Suzuki Kei wakitokea Magomeni kuelekea Temeke, Kijichi mpaka eneo ulipokutwa mwili wa marehemu".
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: [ Ссылка ]...
HabariLeo: [ Ссылка ]
DailyNews: [ Ссылка ]
INSTAGRAM;
HabariLeo: [ Ссылка ]...
SpotiLeo: [ Ссылка ]...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: [ Ссылка ]
MBARONI KWA KUMUUA RAFIKI YAKE NA KUMWIBIA MILIONI 61
Теги
ccmayo tvmillard ayoayotvmtanzaniadigitalmwananchidigitalharmonizetundulisuwasafi tvsimba tvazam tvhellen showstbc onlinehaji manarayanga scmanchester unitedliverpoolzuchuclouds tvkassim majaliwawaziri mkuuikulu mawasilianoflaviana matataMaalim SeifCoronaJPMDK Magufulispika NdugaiMama SamiaTulia AksonBungeni DodomaDiamond PlatnumzHarmonizeKTNTundulisuZitto KabweAli KibaZuchuCCMChademaSamiaSuluhuUchaguzi