Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) una jukumu la kuihakikishia nchi usalama wa chakula kwa kununua na kuhifadhi akiba ya chakula na kutoa chakula cha msaada kwa waathirika waliokumbwa na majanga mbalimbali ya Kitaifa.
#NFRA hutekeleza majukumu yake nchi nzima kupitia kanda nane ambapo mazao yanayonunuliwa na kuhifadhiwa kwa sasa ni mahindi, mtama na mpunga. NFRA ina uwezo wa kuhifadhi tani 341,000 kwa kutumia maghala na vihenge vya kisasa.
#Ununuzi hufanyika kupitia vituo vya ununuzi vya Wakala na vikundi/vyama vya wakulima. Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Wakala umepanga kununua ¹tani 100,000 za nafaka.
#Wakala huzungusha sehemu ya akiba ya chakula kwa kuuza ndani na nje ya nchi kwa lengo la kuhakikisha kuwa chakula kinachohifadhiwa hakiharibiki, kupata nafasi ya uhifadhi katika maghala na kupata fedha za ununuzi wa akiba mpya.
#Kwa mwaka wa fedha 2022/2023, Wakala umepanga kuzungusha takriban tani 124,000 za nafaka.
*MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YA WAKALA*
#Serikali ya Awamu ya Sita imewezesha Wakala kuongeza uwezo wa kununua akiba ya kutosha ya chakula kila mwaka. Kumekuwa na ongezeko la ununuzi kutoka takriban tani 58,000 kufikia zaidi ya tani 110,000 za nafaka kwa mwaka 2021/2022.
#Ununuzi wa nafaka kwa msimu wa mwaka 2022/2023 unaendelea kupitia kanda za Sumbawanga (mikoa ya Rukwa na Katavi), Songea (mkoa wa Ruvuma), Arusha (mkoa wa Manyara), Shinyanga (mkoa wa Kigoma), Makambako (mikoa ya Iringa na Njombe), Songwe (mikoa ya Songwe na Mbeya) na Dodoma.
#Serikali ya Awamu ya Sita imeimarisha hifadhi ya chakula nchini kwa kuongeza akiba ya chakula inayohifadhiwa na Wakala kuwa zaidi ya mara mbili ya kiasi kilichokuwa kinahifadhi kipindi cha miaka mitatu ya hivi karibuni.
#Ongezeko la hifadhi ya chakula imewezesha Wakala kuwa na akiba ya kutosha ya chakula kwa ajili ya kuhudumia kwa wakati mahitaji mbalimbali ya dharura au upungufu wa chakula unaoweza kujitokeza nchini.
#Nchi kwa ujumla ina utoshelevu wa chakula, Wakala umefanikiwa kukabiliana na makali ya mfumuko wa bei za nafaka katika maeneo yaliyohudumiwa, kwa lengo la kupunguza makali kwa kuongeza upatikanaji wa nafaka katika masoko, hivyo kuleta unafuu katika maisha ya wananchi.
#Wakala unahudumia Halmashauri za Bunda, Sengerema, Geita, Nzega, Liwale, Nachingwea, Longido, Loliondo na Monduli ambapo takriban tani 3,000 zimepelekwa katika maeneo hayo. Wakala kwa niaba ya Serikali umejipanga kuhudumia halmashauri nyingine zinazoweza kuthibitika kuwa na upungufu wa chakula ili kuleta unafuu kwa wananchi.
#Wakala unatekeleza Mradi wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka ambapo mradi huo ukikamilika utaongeza uwezo wa kuhifadhi kutoka tani 251,000 hadi tani 501,000. Kwa sasa NFRA ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.
#Wakala umefanikiwa kukamilisha sehemu ya Mradi na kuongeza uwezo wa kuhifadhi kwa tani 90,000 katika Kanda za Arusha (Halmashauri ya Babati) na Sumbawanga (Sumbawanga na Mpanda). Kukamilika kwa mradi huo kumeongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kutoka tani 251,000 hadi tani 341,000.
#Utekelezaji wa mradi katika maeneo mengine Dodoma, Songea, Shinyanga, Songwe na Makambako umefikia asilimia 85.
#Serikali imewezesha NFRA kuimarisha uchumi wa makundi mbalimbali yakiwemo ya Wakulima, Vyama vya Ushirika, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla kupitia mapato yanayopatikana kwa kuuza nafaka kwa NFRA, hivyo kuwa soko la uhakika kwa wakulima.
#Wakala umekuwa ukinunua nafaka kwa bei nzuri, hivyo kuwa soko tegemezi kwa wakulima wengi na kuwapa motisha wakulima kujishughulisha na Kilimo.
#Wakala inachangia mapato ya Halmashauri na Serikali Kuu kupitia utekelezaji jukumu la ununuzi, uhifadhi na uzungushaji wa akiba ya chakula pia unachangia mapato kupitia malipo ya ushuru wa mazao (crop Cess) wakati wa ununuzi/mauzo ya nafaka na ukusanyaji wa kodi ya zuio (Withholding Tax) kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
#NFRA imefanikiwa kuongeza fursa za kiuchumi kwa sekta mbalimbali kupitia kazi za usafirishaji, ununuzi wa vifaa mbalimbali vya uhifadhi na viuatilifu. NFRA hutoa ajira za muda mfupi kwa wananchi zaidi ya 3,000 zinazochangia kuongeza kipato kwa wananchi.
MIKAKATI YA WAKALA KWA MWAKA 2022/23
#Ili kuendelea kuihakikishia nchi usalama wa chakula, Wakala una mikakati ya kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka, kukamilisha Mradi wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka unaoendelea kutekelezwa, kuboresha miundombinu ya uhifadhi, kuendelea kutoa elimu kwa wadau kuhusu uhifadhi bora wa nafaka, kuimarisha mifumo ya kiutendaji na kujengea uwezo watumishi katika nyanja mbalimbali.
#Wakala umejipanga kuhudumia kata, wahifadhi akiba ya kutosha ya chakula kipindi cha mavuno na kuuza chakula pale wanapokuwa na ziada katika uzalishaji.
#rsmmediaNewsUpdates
#youtubersmmedia
Ещё видео!