WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza watumishi wa Halmashauri ya wilaya Mlele wahamie mara moja kwenye nyumba 11 zilizokuwa za wajenzi wa barabara ya Inyonga-Mlele na kukabidhiwa kwa Halmashauri hiyo.
Watumishi ambao ameagiza wahamie kwenye nyumba hizo ni Afisa Usalama wq Wilaya (DSO), Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Mlele {OCD}, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele, Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini {TARURA} Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mlele {DMO} pamoja na watumishi wengine wa hospitali ya wilaya.
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana {Desemba 13, 2022} wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mlele mkoani Katavi baada ya kujionea mwenyewe kuwa zimetelekezwa na zinaharibika kwa kukosa uangalizi.
Nyumba hizo 11 zenye ukubwa tofauti kati yake mbili zinauwezo wa kuchukua familia nne kila moja ni za kisasa na zilikabidhiwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mlele Novemba 2022 na Wakala wa Barabara Tanzania {TANROADS} baada ya kukamilika kwa mradi wa barabara.
Ещё видео!