Mvulana wa miaka 14 aliyepigwa risasi kumi na moja za mpira na maafisa wa usalama kwenye maandamano ya kupinga mswada wa fedha jijini Nakuru, ameendelea kuhangika na maumivu. Licha ya kuondolewa hospitalini siku tano zilizopita, kijana huyu amesalia na risasi tano mwilini. Na kama Maryanne Nyambura anavyoarifu, familia ya mwanafunzi huyu wa kidato cha kwanza imewachwa na mzigo wa kumtibu kijana huyu baada ya madaktari kuelekezea hatari ya kutoa risasi zilizosalia
![](https://i.ytimg.com/vi/HJl04b-ADT0/maxresdefault.jpg)