Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Abdallah Bulembo amesema anaweza kwenda Mahakamani endapo kama Katiba ya TFF haikubadilishwa hususani katika kipengele cha Elimu kwa mgombea Urais.
Bulembo amesema kuwa Katiba ya TFF ambayo inamtaka mgombea urais ama umakamu awe na elimu ngazi ya Digrii inakinzana na Katiba ya Nchi, FIFA na CAF ambazo hazijaweka ukomo wa Elimu.
Bulembo ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam ambapo pia amesema kuwa endapo kama mabadiliko hayajafanyika kabla ya uchaguzi atakwenda mahakamani.
![](https://i.ytimg.com/vi/IFcnyvMhR_U/mqdefault.jpg)