Al Kaaba au jina jingine (Bayt Allah) yaani nyumba ya Mungu kwa mujibu wa Wikipedia ni jengo jeusi, lenye umbo la mraba (pembe nne sawa). Ni nyumba ya kale ya ibada iliyojengwa na Makureysh kipindi cha kabla ya Uislamu. Iko katika mji wa Makka kwenye nchi ya Saudi Arabia leo. Kila mwaka Waislamu mamilioni huenda kufanya Hijja kwenye Al Kaaba hiyo, iliyomo ndani ya Msikiti wa Masjid al Haram uliopo Makka.
Waislamu leo, huamini kwamba, sala moja katika msikiti huo ambao ndani yake ndimo mlimo na Al kaaba ni bora mara 1,000 zaidi ya misikiti mingine, isipokuwa ule wa Madina na kwa mbali ule wa Yerusalemu (Masjid Al Aqsa).
Jengo hilo limezua utata mkubwa sana wa kiimani kwa Waislamu wenyewe kwa wenyewe, watu wa imani zingine zisizo za Kiislamu, na kwa wana historia pia. Utata huo unasababishwa na ile dhana ya kabila la Makureysh (kabila la Mtume wa Waislamu Muhammad) kuzusha kwamba na wao pia ni watoto wa Ibrahim, kama walivyolieleza jambo hili katika vitabu vyao sahihi na vinavyoaminika. Karibu tujifunze….!
![](https://i.ytimg.com/vi/JOzc44JsGCs/maxresdefault.jpg)