#newsarea #trendingex #habarizote #tucta
Serikali imeanza Mazungumzo na Viongozi wa shirikisho la vyama vya Wafanyakazi Nchini Pamoja na Viongozi wa vyama vinavyounda Shirikisho hilo Jijini Dodoma Kwaajili ya kujadili Juu ya sintofahamu iliyojitokeza katika ahadi ya Nyongeza ya Mshaara ya Asilimia 23.3 kwa wafanyakazi iliyoanza kutekelezwa mwezi Julai.
Akizungumza Raisi wa Shirikisho la Vyama vya wafanyakazi TUCTA Tumaini Nyamhokiya amesema wamewasilisha malalamiko yao kwa Serikali kwani Kiwango cha Nyongeza ya Mshahara iliyoongezwa katika Mwezi Julai ni kinyume na ahadi iliyotolewa na Rais Samia siku ya Mei Mosi mwaka huu kwani baadhi ya watumishi wamepata nyongeza ya shilingi Elfu Nane na kuendelea.
![](https://i.ytimg.com/vi/JdNXosIZDh4/maxresdefault.jpg)