Jeshi la Polisi mkoa wa Kigoma, linamshikilia Arving Bagisheki (39),kwa mahojiano baada ya kukutwa na nyara za serikali meno ya tembo mawili ndani ya gari.
Akizungumza leo, Julai 3,2024 Kaimu Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Kigoma, Iddi Kiyogomo amesema tukio hilo limetokea Julai mosi, 2024 majira ya saa 4:00 usiku, katika eneo la Kihomoko kwenye kizuizi cha polisi barabara ya ya Kibondo/Kakonko wilayani Kakonko.
![](https://i.ytimg.com/vi/K4BynVw_wYI/maxresdefault.jpg)