Vikao vya wabunge vilivyokuwa vimetibuka mjini Mombasa vimeanza rasmi leo baada ya kususia vikao kwa siku tatu. Wabunge kupitia kamati mbali mbali wanaangazia makadirio ya bajeti pamoja na deni la taifa ambalo wanasema limekuwa mzigo mkubwa na kuhujumu maendeleo. Mwenyekiti wa kamati ya bajeti Ndindi Nyoro pamoja na naibu mwenyekiti katika kamati ya deni na uwekezaji makali mulu wamedokeza kuwa serikali inalenga kufunga mashirika ya serikali ambayo hayaleti faida kwa serikali ili kupunguza mzigo kwa wakenya.
Ещё видео!