Huwezi kuwazungumzia Wahehe ukaeleweka vizuri bila kumtaja Chifu wao, Mkwawa.
Chifu Mkwawa alizaliwa mwaka 1855, akapewa jina la Ndesalasi, maana yake ikiwa ni “mtundu au mdadisi”.
Historia inaonyesha kuwa alizaliwa katika kijiji cha Luhota, Wilaya ya Iringa na kwamba jina la Mkwawa linatokana na neno Mkwavinyika likimaanisha ‘mshindi wa nchi nyingi’.
Sifa kubwa ya Mkwawa ilikuwa ni nguvu na uwezo wake wa kupigana vita.
Simulizi zinaonyesha kuwa ukubwani, miaka ya 1887 Mkwawa pia aliitwa ‘Mtwa Mkwava Mkwavinyika Mahinya Yilimwiganga Mkali Kuvago Kuvadala Tage Matenengo Manwiwage Seguniwagula Gumganga’.
Jina hilo linamaanisha ni “Mtawala, mtekaji wa nyika, mkali kwa wanaume, mpole kwa wanawake asiyetabirika, aliyeshindikanika, mbabe mwenye nguvu, udongo pekee ndio utakaomuweza”.
Ещё видео!