Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye amewasili katika Ofisi za Wizara hiyo zilizopo katika Mji wa Serikali Mtumba na kupokelewa na Menejimenti na watumishi wa Wizara hiyo wakiongozwa Naibu Waziri wake Mhandisi Kundo Mathew na Katibu Mkuu Dkt. Jim Yonazi mara baada ya kuapishwa Ikulu ya Chamwino jana tarehe 10.01.2022 baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri na watendaji wakuu Wizara katika ngazi ya Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu.
Mhe. Nape amezungumza na watumishi wa Wizara hiyo na kuwataka kufanya kazi kwa bidii, weledi na utulivu ili kuwezesha Sekta mbalimbali kupitia huduma za mawasiliano na TEHAMA pasipo urasimu na hatimaye nchi izidi kusonga mbele na Wizara yake iwe ni Wizara ya mfano katika kusukuma gurudumu la maendeleo ya nchi.
MAPOKEZI YA WAZIRI NAPE NNAUYE OFISINI KWAKE, WATUMISHI WA WIZARA WAMPOKEA...
WATCH WASAFI TV📺
AZAM - 411 | DSTV - 296 | ZUKU - 028 | STAR TIMES - 444 & 333 | COCONUT TV - 20 | DODOMA CABLE - 113
LISTEN WASAFI FM 📻
88.9 DAR/ZNZ/PWANI 📻 | 104.1 DODOMA 📻 | 94.5 ARUSHA 📻 | 97.3 MBEYA 📻 | 94.9 MWANZA 📻 | SHINYANGA 106.3 📻 | KIGOMA 101.7 📻
Follow Us On:
INSTAGRAM: [ Ссылка ] || [ Ссылка ]
TWITTER: [ Ссылка ] || [ Ссылка ]
FACEBOOK: [ Ссылка ]
𝑪𝒐𝒑𝒚𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕 ©2021 𝑾𝒂𝒔𝒂𝒇𝒊 𝑴𝒆𝒅𝒊𝒂. 𝑨𝒍𝒍 𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕𝒔 𝒓𝒆𝒔𝒆𝒓𝒗𝒆𝒅.
#wasafi #wasafitv #wasafifm
Ещё видео!