Rais Samia Suluhu Hassan amerejesha utaratibu wa nyongeza ya mshahara kwa watumishi wa umma ya kila mwaka ambao ulisitishwa kwa muda mrefu na ameahidi nyongeza hiyo itaanza kutolewa mwaka huu wa 2023.
Rais Samia aliyekuwa akizungumza leo Mei Mosi 2023 mkoani Morogoro katika sherehe za maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani amesema utaratibu huo utaanza mwaka huu.
“Niseme pia kuna nyongeza za mishahara kwa mwaka ambazo kwa muda mrefu zilikuwa zimesitishwa nikaona mwaka huu tuzirudishe.
“Kwa hiyo wafanyakazi wote mwaka huu mbali niliyoyasema lakini kuna nyongeza za mishahara kila mwaka na tunaanza mwaka huu na tutaenda kila mwaka kama ilivyokuwa hapo zamani,” amesema Rais Samia.
Hata hivyo, kiongozi huyo mkuu wa nchi amesema Serikali haiwezi kutaja hadharani nyongeza hiyo ya mshahara ili kuepuka kupanda kwa bei ya bidhaa mbalimbali sokoni kunakowezwa kufanywa na baadhi ya watu.
“Kile watu walichozoe tukisema hapa ili wapandishe bei madukani mara hii hakuna tunakwenda polepole kupandishana kama tulivyosema, wasione tumeongezeana kitu gani ili mwenendo wetu wa bei uwe salama,” amesema Rais Samia.
Amewataka wafanyakazi kutokuwa na wasiwasi kwa sababu “mambo mazuri yapo lakini hatutayatangaza hapa (kwenye sherehe za Mei Mosi) lakini wafanyakazi mambo ni moto, mambo ni fire.”
Soma: [ Ссылка ]
Twitter: [ Ссылка ]
Facebook: [ Ссылка ]
Subscribe kwa makala zaidi za kina na kiuchambuzi @Nukta TV
![](https://i.ytimg.com/vi/MDICYhQzDiw/maxresdefault.jpg)