Simba SC imepata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya KMC, katika mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa leo kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
KMC wametangulia kupata bao kupitia kwa Hassan Kabunda dakika ya 41 kabla ya Simba kuchomoa kwa goli la Kibu Denis dakika ya 52, kasha Pape Sakho akaongeza la pili dakika 63 na Henock Inonga akafunga hesabu dakika ya 66.
![](https://i.ytimg.com/vi/MIisXjiothY/maxresdefault.jpg)