Rais Mteule William Ruto amefanya mazungumzo ya moja kwa moja ya njia ya simu na rais anayeondoka Uhuru Kenyatta. Ruto kwenye mtandao wake wa Twitter amesema, mazungumzo yao yamegusia uchaguzi mkuu uliopita na shughuli ya mpito inayaotarajiwa kutoa madaraka kutoka kwa rais Kenyatta hadi kwa rais mteule Ruto. Mazungumzo haya yakifanyika siku mbili baada ya mahakama kuafiki ushindi wa Ruto kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti tisa. Mazungumzo ya Rais Uhuru na naibu wake yakijiri baada ya kile rais mteule ameyataja kuwa ya kwanza katika muda wa miezi kadhaa
![](https://i.ytimg.com/vi/MOwcm93_xMk/maxresdefault.jpg)