Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema kuwa serikali haijazuia uuzaji wa mahindi nje ya nchi, bali inawataka wanunuzi wa nje kufuata utaratibu maalumu, ikiwemo kujisajili nchini ili kuondoa viashiria vyote vinavyoshabihiana na unyonyaji kwa mkulima ikiwemo kuwatumia madalàli kuvusha mazao katika mipaka ya nchi.
Bashe ametoa kauli hiyo leo Juni 22 baada ya Mbunge wa Mbozi George Mwenisongole, kulitaka #Bunge kuahirisha ratiba iliyopo ili kujadili suala la Bei ya mahindi ambayo amesema ipo katika hali mbaya na haioneshi mwelekeo wa kumsaidia mkulima.
Bashe amesema Serikali imeshatoa fedha kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula #NFRA kununua zao hilo kwa wakulima ambapo makao makuu ya vituo vya mkoa kilo ya mahindi inanunuliwa kwa shilingi mia nane (800) huku vituo vya ndani ya mkoa kilo ikinunuliwa kwa Tsh. Mia sita (600) na fedha hizo za ununuzi zimefika katika maeneo husika ukiwemo mkoa wa #Njombe , #Rukwa , #Mbeya na #Iringa
#kingsfmradio #jisikiemfalme #NipoTayari #Dodoma
![](https://i.ytimg.com/vi/MSI9Xas9Yco/mqdefault.jpg)