Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Albert Chalamila amewataka Watendaji wa Serikali kutoka TANROADS, TARURA, DAWASA, UDART pamoja na TRC kuhakikisha wanakuwa na mpango kazi wa Pamoja ambao utakwenda kuondoa Tatizo la Kutuama kwa Maji machafu yanayotokana na mvua kwenye maeneo ambayo miradi yao inapita hususani katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
RC Chalamila ametoa kauli hiyo leo Juni 12, 2023 Jijini Dar es Salaam wakati wa Ziara yake iliyolenga kukagua miundombinu ambayo imekuwa na Kasumba ya Kutuamisha na kutiririsha maji hasa nyakati za mvua, Suala ambao imekiwa ni kero kwa Wakazi wa Jiji hilo.
"Haiwezekani mheshimiwa Rais anapita maji yaliyotuama yanapiga kwenye kioo cha Gari lake..Meneja wa Tanroads upo, Meneja wa Tarura Upo, Meneja wa Dawasa Upo, Je tumekubaliana na hiyo hali au tufanye kitu gani?" amesema RC Chalamila.
![](https://i.ytimg.com/vi/M_uyJhAqp9s/mqdefault.jpg)