DR. MAKAME KAIMU SPIKA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI
Mbunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) kutoka Tanzania, Dr. Abdullah Makame Alhamis hii ameongoza kikao cha Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha, ambapo bunge hilo linaendelea na vikao vyake.
Dr. Makame alichaguliwa na Wabunge wenzake kwa kura zote kukaimu nafasi ya Spika, kufuatia Spika wa Bunge hilo Mheshimiwa Martin Ngoga kusafiri kikazi nje ya Nchi.
Kutokana na muundo wa Bunge la Afrika Mashariki, nafasi ya Spika haina Naibu Spika, hivyo kanuni zinaelekeza kuwa iwapo Spika akipata dharura wakati vikao vya Bunge vinaendelea, atachanguliwa Mbunge mmoja wa bunge hilo kwa kupigiwa kura, kukaimu nafasi ya Spika na kuongoza vikao.
Kwa sasa Bunge hilo lina jumla ya Wabunge 54 kutoka Nchi wanachama wa Jumuiya hiyo, ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Sudan Kusini, ambapo mwanachama mpya wa Jumuiya hiyo, Congo DRC haijachagua wabunge wa kuiwakilisha.
#eacparliarment #aicc
![](https://i.ytimg.com/vi/Mw8yrX1FkIU/mqdefault.jpg)