Dar es Salaam. Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, imesema imeingia mkataba na kampuni watengenezaji wa mashine za tiba-mionzi, wanayolipia kiasi cha Dola za Marekani 210,934.44 sawa na Sh600 milioni kila mwaka.
Kwa mujibu wa stakabadhi ambazo mwandishi aliziona ni zile zilizolipiwa kwa kipindi cha mwaka 2023 na 2024, zinazoonyesha makubaliano kwamba mzalishaji wa mashine hizo anapaswa kuzifanyika matengenezo kinga mara mbili kwa mwaka na atatakiwa kutengeneza ndani ya saa nne (4) ikiwa itaharibika.
Hayo yamesemwa mapema wiki hii na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dk Julius Mwaiselage alipozungumza na gazeti hili, wakati akitolea ufafanuzi ripoti maalum iliyochapishwa na gazeti hili kuhusu changamoto za huduma za tiba za mionzi hospitalini hapo.
Ripoti hiyo iliyochapishwa kuanzia Juni 24, iliangazia upungufu wa vifaa tiba vya saratani ocean road, unavyochelewesha muda wa kupata matibabu ya tiba mionzi kwa wagonjwa na kusababisha vifo vinavyoweza kuepukika.
![](https://i.ytimg.com/vi/MzT_6ePiRxg/maxresdefault.jpg)