Sheikh wa Mkoa wa Singida Issa Nassoro Issa ametoa tahadhari kwa Waislam mkoani hapa kuhusu suala ambalo limeanza kuibuka la mapenzi ya jinsia moja.
Issa alitoa taahadhari hiyo jana wakati akizungumza na waislam wa Msikiti wa Taqwa mjini hapa baada ya swala ya magharibi kufuatia kuwepo kwa baadhi ya taasisi za kidini na mashirika mbalimbali kuanza kuhamasisha ya ushoga kwa kutoa misaada ya vitu mbalimbali vyenye nembo zinazohamasisha mapenzi ya jinsia moja (ushoga) ikiwemo misaafu.
"Ndugu zangu waislam tuchukue tahadhari ya hii ya misaada tunayopewa kwani mingine imewekwa alama za kuhamasisha ushoga hivyo kabla ya kupokea misaada yoyote ni lazima ifanyiwe uchunguzi" alisema Sheikh Issa.
![](https://i.ytimg.com/vi/NBAO6ZQAj7M/maxresdefault.jpg)