Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara leo wameangukia pua baada ya kuchapwa bao 1-0 na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.
Bao la Kagera kwenye mchezo wa leo limepatikana baada ya beki wa Simba Mohamed Hussein Zimbwe Jr kujifunga dakika ya 42 wakati akijaribu kuokoa hatari langoni mwake baada ya kuchanganyana na kipa wake Aishi Manula.
Ushindi huo ni mwendelezo wa ubabe wa timu hiyo kutoka mkoani Kagera kwa Mnyama Simba, baada ya awali kuipa kichapo cha mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Kaitaba Bukoba katika mchezo wa kwanza msimu huu.
Matokeo hayo yameineemesha Kagera Sugar katika jitihada za kuepuka kushuka daraja, ikifikisha pointi 43 na kukaa nafasi ya 10 huku Simba wakisalia kileleni na pointi 81.
Ещё видео!