MANYARA: ALIYEUA MKE NA MTOTO AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA...
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Manyara imemuhukumu Shamswadini John (35) mkazi wa Hanang mkoani Manyara kunyongwa hadi kufa baada ya kukutwa na hatia ya kuua kwa kukusudia ambapo amemuua mke wake aitwaye Asia John (25) na mtoto wake, Ahmedi Shamswadini (09).
Hukumu hiyo imetolewa Desemba 7,2022 na Jaji Devotha Kamzola ambapo amesema mshtakiwa Shamswadini alimuua mke wake kwa kumnyonga ambapo wakati akitekeleleza mauaji hayo mtoto alikuwa akipiga kelele hivyo baada ya kumuua mama akarudi kumuua na mtoto.
Ameeleza mahakamani hapo kuwa, baada ya kufanya mauaji hayo, Shamswadini alichimba shimo na kuufukia mwili wa mke wake, lakini alipotaka kuufukia mwili wa mtoto alishindwa kufanya hivyo kwa kuhofia kuwa kumeshaanza kukucha na watu watamuona hivyo akaamua kwenda kuutupa mwili wa mtoto katika bwawa ili kupoteza ushahidi.
Uchunguzi wa daktari umeonesha ni kweli wamefariki dunia kwa kukosa hewa baada ya kunyongwa huku Wakili wa Serikali Petro Ngassa akiiomba mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hizo.
Muuaji alifanya tukio hilo Oktoba 31, 2018 huko katika Kijiji cha Hideti wilayani Hanang huku chanzo cha mauaji hayo kikiwa ni ugomvi uliotokea mara baada ya mwanaume kuongeza mke wa pili jambo lililomchukiza mke wa kwanza na kuamua kuhama nyumba ambapo aliamua kwenda kupanga chumba na kuanza kuishi na mtoto wake.
⚫️ SIKILIZA + 255 GLOBAL RADIO LIVE: [ Ссылка ]
⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:
⚫️ ANDROID:[ Ссылка ]
⚫️ iOS:[ Ссылка ]
⚫️ VISIT COMEDY PLAYLIST: [ Ссылка ]
⚫️ JE, NA WEWE UNA HABARI?
⚫️ WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE: ( +255 657 693 210), ( +255 713 750910)
⚫️ Email: globaltvonlinenews@gmail.com OR abbymrisho@gmail.com
⚫️ OUR PLAYLISTS:
⚫️ MICHEZO na BURUDANI: [ Ссылка ]
⚫️ HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA: [ Ссылка ]
⚫️ GLOBAL RADIO TV: [ Ссылка ]
⚫️ EXCLUSIVE INTERVIEW: [ Ссылка ]
⚫️ Subscribe Global TV [ Ссылка ]
![](https://i.ytimg.com/vi/NKooEpXxIVc/maxresdefault.jpg)