Kufuatia Rais wa Marekani Joe Biden kutangaza kubwanga manyanga kwenye mbio za kuwania urais kwa awamu ya pili, na hivyo kumpndekeza Makamu wake Bi. Kamala Devi Harris kupeperusha bendera ya chama cha Democrats, rasmi sasa Kamala ameanza kampeni siku ya Jumatatu, Julai 22, 2024 alipozungumza na wafuasi wa Democrats makao makuu ya timu ya kampeni.
Katika hotuba yake Kamala alijigamba kuwa anao uwezo wa kumshinda mpinzani wao Donald Trump ambaye alimtuhumu kwa kashfa nyingi ikiwemo kesi zinazomkabili Rais huyo wa zamani wa Marekani.
Houtuba hiyo ya Kamala mwenye umri wa miaka 59 inakuja wakati tayari nyota njema imeanza kuonekana, kwani amekuwa na upepo mzuri muda mfupi tangu Joe Biden atangaze kung’atuka kufuatia shinikizo la vigogo wa Democrats.
Unaweza kutufuatilia kupitia;
TWITTER: [ Ссылка ]
INSTAGRAM: [ Ссылка ]
FACEBOOK: [ Ссылка ]
TIKTOK: [ Ссылка ]_...
Au tembelea tovuti yetu: [ Ссылка ]
Je, una habari? wasiliana nasi kupitia Telegram/WhatsApp +255 753 815 105
The Chanzo Initiative, 2024 © All Rights Reserved.
Ещё видео!