Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema taarifa iliyotolewa na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) kuhusu muswada wa marekebisho ya sheria ya huduma za habari namba 12 ya mwaka 2016, imelenga kujenga chuki kwa waandishi wa habari na Serikali.
Nape amesema taarifa hiyo pia imeonyesha Serikali kuwa vipande vipande kwa kuonesha kuwa baadhi ya viongozi wanataka marekebisho hayo na wengine hawataki.
Waziri Nape ameyasema hayo leo Februari 9, 2023 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.
![](https://s2.save4k.ru/pic/O3MCPgx9kyw/maxresdefault.jpg)