Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Martin Ngoga, amemuapisha James Kakooza kuwa mbunge wa bunge la Afrika Mashariki, uapisho uliofanyika kwenye bunge hilo lililoendeshwa jijini dar e salaam, huku baadhi ya wabunge wakishiriki kwa njia ya mtandao kutoka kwenye nchi zao.Uapisho wa Bwana Kakooza kutoka nchini Uganda unafuatia kifo cha mmoja wa wabunge tisa wa bunge hilo ambao wanatoka nchini Uganda.
Mara kiapo hicho Spika wa Bunge hilo mbunge huyo alikabidhiwa zana za kazi ambazo zitamuongoza katika kutimiza majukumu yake ya ubunge wa afrika mashariki. Wakizungumzia tukio hilo baadhi ya wabunge wamesema
Bunge la Afrika mashariki linaundwa na wabunge kutoka nchi sita wanachama wa jumuiya hiyo, ambapo kila nchi inatoa wabunge tisa na mawaziri wa mambo ya nje pamoja na manaibu wao kutoka nchi wanachama ambao wanaingia moja kwa moja kwa mujibu wa sheria na hivyo kufanya bunge hilo kuwa na jumla ya watu 66
![](https://i.ytimg.com/vi/OmkiaoYyGgA/maxresdefault.jpg)