#GLOBALHABARI
GLOBAL HABARI SEPT 22: Idadi ya Waliofariki MV Nyerere Yaongezeka!
Kufuatia vifo vya watu zaidi ya 190 waliofariki kwa ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV. Nyerere katika kisiwa cha ukara wilayani Ukerewe, wakati zoezi la uokoaji likiendelea mhandisi wa kivuko hicho Alphonce Augustino Cherehani ameokolewa akiwa hai mapema leo asubuhi.
Akizungumza baada ya kuokolewa mmoja waliokuwa katika kivuko hicho ameelezea chanzo cha ajali hiyo
Insert ….. Mchori Bulola- Aliyeokolewa
Pia kikosi cha uokoaji kimeelezea mikakati iliyowekwa ili kufanikisha zoezi hilo la uokoaji.
Kutokana na msiba huo kwa taifa Kampuni ya mawasiliano Tanzania Vodacom imetoa msaada kiasi cha shilling million 10 kwa serikali kwaajili yakufanikisha shughuli za mazishi kwa watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo
Katika hatua nyingine waziri wanchi ofisi ya waziri Mkuu anayeshughulikia maafa Jenista Mhagama amesema kuwa mfuko maalum utatengenezwa ili kuweza kupokea michango ya rambirambi itakayoweza kufanikisha mazishi ya waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
Insert:Jenista Mhagama- waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuus
Hata hivyo baada yakutokea ajali hiyo viongozi mbalimbali wamefika katika eneo la tukio ikiwa ni pamoja na waziri mkuu Kassim Majaliwa, waziri wanchi ofisi ya waziri Mkuu anayeshughulikia maafa Jenista Mhagama, mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama IGP Simon Sirro, mkuu wa mkoa mwanza John Mongela, waziri wa mambo ya ndani Kangi Lugola, Mkuu wa Mkoa wa mara, Mbunge wa ukerewe na wengine.
://bit.ly/2AAQe1d iOS: [ Ссылка ] Subscribe [ Ссылка ] FACEBOOK: [ Ссылка ]... TWITTER: [ Ссылка ] Visit [ Ссылка ], Suazi1 [ Ссылка ] WEBSITE:
[ Ссылка ] FACEBOOK: [ Ссылка ]... TWITTER: [ Ссылка ] INSTAGRAM: [ Ссылка ].
Ещё видео!