Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Katavi imemuhukumu kunyongwa hadi kufa Shija Sosoma mkazi wa kijiji cha Mawiti wilaya ya Mlele baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumuua kwa kukusudia mkewe, Ng'washi Nkuba.
Ilielezwa mahakamani hapo kuwa tukio hilo limetokea mwaka 2012.
Hukumu hiyo ilitolewa jana June 30, 2020 na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga, David Mrango baada ya upande wa mashtaka kuthibitisha.
Jaji Mirango amesema mshtakiwa ametenda kosa kinyume cha sheria ya kanuni ya adhabu kifungu cha 196.
Amesema alimchoma mkewe kisu shingoni na sehemu mbalimbali za mwili kwa madai kuwa alimuua mtoto wa mke mwenza kwa imani za kishirikina.
Wakili wa Serikali, Lugano Mwasubi akizungumza na waandishi wa habari nje ya mahakama ameishukuru mahakama kwa kutenda haki, kwa kuwa vitendo vya namna hiyo havikubaliki katika jamii.
UTATA MWANAMKE ANAYEDAIWA KUUAWA NA MUMEWE DAR
[ Ссылка ]
Ещё видео!